Tuesday, 10 October 2017

HISTORIA.

HISTORIA YA WATUMISHI SINGERS.

SHUKRANI;
Tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa Bwana wetu Yesu Kristo ,kanisa kwa ujumla kwa maombi yenu pamoja na wafadhili wetu waliotufadhili kwa njia moja au nyingine. Mungu awabariki sana.
KUANZA KWA KIKUNDI
Wazo hili la kuanzisha kikundi cha injili kwa njia ya uimbaji lilitoka baina ya familia mbili ambazo ni familia ya Magita Mataro na Kasoga Kasika mnamo mwaka 2015 na kushiriki katika huduma mbalimbali za kanisa kwa nafasi zilizoweza kupatikana.
Ilipofika mwaka 2016 wazo liliwapendeza pia baadhi ya marafiki katika familia hizi mbili na kuamua kujiunga ili kuitenda kazi kwa nguvu zaidi. Mwezi septemba 2016 kikundi kilisajiliwa rasmi katika kanisa kikiwa na jumla ya waimbaji saba. Zoezi la usajili wa waimbaji liliendelea mpaka kufikia waimbaji 13.
MALENGO YA KIKUNDI
Kikundi kilianzishwa kikiwa na malengo yafuatayo:-
·         Kufanya kazi ya injili kwa njia ya uimbaji, mikutano ya injili na huduma mbalimbali za kijamii na kiroho pia.
·         Kufanya shughuli za ujasiriamali ili kupata kipata kufanikisha malengo ya kikundi.
MAFANIKIO
·         Kwa kutumia michango yetu wenyewe tumefanikiwa kurekodi santuri ya sauti (Audio CD) iliyotugharimu takribani shilingi 1,500,000/= yenye jina la KESHENI.

·         Tumefanikiwa kutembelea kwa kusudi injili na kuomba na familia mbalimbali ndani na nje ya kanisa.

No comments:

Post a Comment

KARIBU KUSHIRIKI MBARAKA HUU